DJ JOH wa 93.1 Marekani acheza Ngoma za Diamond! - FARMERCIST 254

FARMERCIST 254

This site discusses farming issues in relation to Kenya with particular emphasis on poultry farming.

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday 19 July 2016

DJ JOH wa 93.1 Marekani acheza Ngoma za Diamond!

Haya sasa naona taratibu ule ubishi wa kuwa nyimbo za Afrika hasa Tanzania hazichezwi kwenye vituo vya Radio za Marekani unaelekea kuisha! Dj Joh wa 93.1 Marekani akihojiwa na Millard Ayo amezungumzia nafasi ya wasanii wa Afrika kusika katika vituo vya Radio vya marekani!! Amelezea Mengi lakini amekiri mara ya kwanza ili apate hiyo kazi ilibidi adanganye na alikataa kuwa yeye si mtanzania kutokana na ubaguzi lakini baadae alikuja kukubari kuwa ni mtanzania baada ya kazi zake kuanzwa kupendwa! Alienda Marekani kwa ajiri ya kusoma lakini alifika hatua akaanza kuwa Dj lakini hakuruhusiwa kuplay nyimbo za kiafrika kwani hakuwa anaruhusiwa!! Anasema yeye ni anapenda Afro Pop na anaupenda sana mziki wa Diamond!!!! Kwa mara ya kwanza alijitosa na kuanza kuplay nyimbo za akina P-squre,Wizkid na Diamond!!! Anasema siku hiyo alipokea comments nyingi sanaaa zilizo mpongeza na kufanya yeye kuongeza juhudi ya kuplay nyimbo za kiafrika hasa Za diamond Anasema siku ambayo hatoisahau ni siku Alio play nyimbo za Diamond na baada ya kipindi alipigiwa simu na Mtu ambae ni Mmarekani na alimuuliza kuwa Diamond kamfahamia wapi ndipo Dj Joh alipo sema yeye ni mtanzania na anamfahamu Diamond!!! Yule mmarekani alimwambia yeye Kwa Afrika Diamond ndo Msanii anaye mvutia na kwenye Gari yake muda mwingi huwa anasikiliza nyimbo za Diamond japo haelewi lugha!!! Dj Joh amesema kuwa Yule mmarekani alimwambia wiki ijayo nina harusi yangu na ninaomba uje Uwe Dj kwenye Harusi yangu na Nyimbo za Diamond uwe nazo nyingi!! Hapo Dj Joh anasema alifurahi nakuona kuwa mziki wetu sasa unakuwa!! Dj Joh amesema number don't lie kwani ni wengi walio mpigia simu na kumpongeza na kumtaka kumjua Diamond!!! Mbali na hilo kuna siku Diamond alipost video ilionesha sehemu fulani Marekani watu wapo kwenye shuhuri wakisikiliza Nasema nawe!! Millard ayo ameongeza na kusema kuwa pia kuna kituo kingine cha Radio marekani kinachoitwa CSB nacho hucheza nyimbo Za Diamond!!! Ni wazi sasa mziki wetu umefika mbali!!! Kuna siku niliwahi sema Diamond nyimbo yake na Neyo itachezwa sana kwenye Vituo vya Radio vya Marekani lakini watu walinipinga sana humu na sasa limeanza kujidhihirisha Kabla hata ya hiyo collabo.

For More Music Updates And News FIND US ON:

TWITTER: @King25flow

FACEBOOK: King25flow

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages